Rachel alidai kuwa wakati akisoma udogoni lengo lake kubwa lilikuwa
ni kuja kuwa mwanasheria kwani ndio kazi aliyokuwa akiipenda na aliamini
kwamba ndoto yake ingetimia siku moja.
Lakini mwanadada huyo alisema kila kitu kiliharibika baada ya
kujiingiza katika filamu na kujikuta sasa maisha yake yapo kwenye filamu
zaidi.
Rachel, alisema "Lakini baada ya kuanza kuigiza nikaona watu wananikubali na
kupenda kile nikifanyacho, ndipo nilipoanza kupata mafanikio nikaona OK,
kumbe hii ni kazi, nikaanza kuifanya kwa umakini zaidi,"
Rachel alisema "kimya chake cha muda baada ni kutoka na kuanda filamu mpya ya Kidudumtu ambayo inakaribia kutoka hivi karibuni .alisema nashukuru
Mungu nimemaliza filamu mpya ya Kidudumtu salama na naomba watu waisubirie ujio mpya,"
aliongeza Rachel Njingo.