Kurasa

Ijumaa, 5 Juni 2015

Q-CHILLAH AAHIDI MAKUBWA!


 
Q-Chillah akielezea namna alivyojipanga kwa ujio wake mpya. Kushoto ni Meneja wake, QS. Mhonda. 
 
Muandaaji wa hafla hiyo, DJ Bavon (aliyesimama) akitoa ufafanuzi. 
Msanii wa Bongo Fleva, MB-Dog (kulia) akiwa katika pozi na Q-Chillah kwenye uzinduzi huo.
 
Msanii wa Bongo Fleva, Isabella Mpanda akimmiminia kinywaji mchumba wake, Luten Karama.
 
Wasanii Luten Karama kushoto, Isabella Mpanda katikati pamoja na Baby Madaha wakiwa katika picha ya pamoja.
 
Wageni mbalimbali waliohudhuria hafla hiyo.  
Staa wa Bongo Fleva, Dully Sykes (kulia) akipozi katika picha ya pamoja na wasanii.  
Msanii Rich Mavoko akifuatilia kwa umakini hafla hiyo.
 
Dully Sykes katikati akiwa na wasanii wenzake chipukizi.
 
Wasanii wakiwa katika pozi, wapili kutoka kulia ni Q-Chillah akifuatiwa na Dully Sykes.

MSANII wa muziki wa Bongo Fleva, Abubakar Katwila ‘Q-Chillah’ amesema  hategemei kupotea tena kutokana na ujio wake mpya katika gemu baada ya kupotea kwa muda mrefu.
Q-Chillah ameyasema hayo jana usiku katika Hoteli ya Star City jijini Dar es Salaam alipokuwa akizindua video zake mbili zinazokwenda kwa jina la For U pamoja na Power of Love.
Alisema kwa sasa amefanikiwa kumpata meneja wake mwenye kutambua vipaji vya wasanii hasa katika kuviendeleza akimtaja kwa jina la Joseph Mhonda ambaye pia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya QS. Mhonda.