Msanii ambaye anamiliki shirika la SHUIMA Paskal Linda Mgundu a.k.a Batarokota anatarajia kufanya onyesho kwaajili ya utambulisho wa wimbo wao mpya wa We shetan katika ukumbi wa Pricess Hall uliopo Mombasa nchini Kenya jumatano ijayo.
Akizungumza na Blog hii meneja wa Batarokota hilo Markus James alisema, Batarokota amealikwa nchini Kenya kwa mwaliko wa udhamini wa Op Limited ya jijini Mombasa hivyo anatarajia kutumia ziara hiyo kuzindua songi lake jipya we shetan, Onyesho hilo limedhaminiwa na Stream ii Co. Ltd, G-Unit Music and Commucation na Nyuki Grocery. Baada ya utambulisho na show ya Batokota usiku huo burudani ya muziki itashushwa kutoka kwa Dj Zari, Dj Casto, Dj Peter na Dj Opio huku wasanii waalikwa watakuwa Daz P, Y Bring bring, Mchomoko.Big D wakiwa wasindikizaji alisema